Indirimbo ya 188 mu NYIMBO ZA WOKOVU

1
Wengi wakasema: “Bado”, walipoitwa na Mwokozi, lakini tena wakaona wamechelewa kuokoka.
Njoo mbio, njoo mbio, Yesu akuita leo! Njoo mbio, njoo mbio, usichelewe, ndugu yangu!
2
Nawe usemaye: “Bado”, unapoitwa naye sasa, rafiki, labda utakuta mlango umekwisha fungwa.
3
“Bado leo”, alisema kijana ‘moja kwa ujinga. Usiku alikufa mara, na akaenda hukumuni.
4
“Bado leo”, wamwambia rafiki yako bora, Yesu, Ataondoka kwa huzuni, utafanyaje bila yeye?
5
“Bado leo”, ukumbuke ni neno la hatari kwako! Waweza kupotea pia, kukosa kuingia mbingu.



Uri kuririmba: Indirimbo ya 188 mu Nyimbo za wokovu