Indirimbo ya 59 mu NYIMBO ZA WOKOVU

1
Yesu, ninakutolea, moyo na maisha yangu, niwe mfuasi wako, Safi na mtakatifu.
:/: Mungu wangu, Mungu wangu, nitakase saa hii! :/:
2
E’ Mwokozi, nitakase, unijaze pendo lako. Na maisha yangu yote yawe yako, Bwana wangu!
3
Ninataka kuheshimu wewe, Mkobozi mwema; nifanane nawe, yesu, kati’ watu wa dunia!
4
Nikikaa kimya kwako kama yule Mariamu, nifundishwe nawe, Bwana, sitahangaika tena.
5
Tawi lake mzabibu, ulitunze na ‘safisha, ili kwa uwezo wako litaza’ matunda mengi!



Uri kuririmba: Indirimbo ya 59 mu Nyimbo za wokovu